Kilimanjaro Queens waanza vizuri Rwanda

Baada
ya timu hiyo kufanya mazoezi nchini Rwanda kwa mara ya kwanza, kocha wa
timu hiyo Bakari Shime ameeleza kuridhishwa na hali ya wachezaji wake.
''Wachezaji wote wameshiriki kikamilifu katika mazoezi tuliyofanya
leo/jana kwenye uwanja wa Mumena hapa Nyamirambo na kwakweli yametupa
matumaini ya kurejea na ubingwa wa CECAFA mwaka huu'', amesema Shime.
Aidha Shime ameongeza kuwa yeye na wenzake kwenye benchi la ufundi
ambao ni Kocha msaidizi Edina Lema, Kocha wa makipa Eliuter Mollel,
Daktari Blandina Mnambya na meneja wa vifaa Ester Chabruma wanaamini
kila walichokifanya kabla, kinatosha kuwafanya wafanye vizuri kwenye
michuano hiyo.
Kilimanjaro Queens inayoundwa na wachezaji 20, inatarajia kucheza
mchezo wake wa kwanza kwenye mashindano hayo ya CECAFA dhidi ya wenyeji
Rwanda Alhamis Julai 19.
No comments